Bwawa la Kuogelea Watoto
Bwawa la kuogelea watoto ni sehemu maalum iliyojengwa kwa ajili ya watoto kucheza maji wakiwa katika mazingira salama. Bwawa hili huwa na kina kifupi cha maji kinachofaa kwa watoto wa umri mdogo, na mara nyingi huwekewa vifaa vya burudani kama slaidi, midoli ya kuogelea, na vitu vinavyoelea. Lengo ni kuwapa watoto nafasi ya kufurahia maji kwa usalama huku wakijifunza na kucheza kwa uhuru.
Water Slide
Water slide ni kifaa cha burudani kilichoundwa kama njia ya mteremko inayoteleza, ambapo mtu huketi au kulalia juu yake na kuteleza kwa kasi hadi kufikia sehemu yenye maji,
Vifaa Vya Michezo ya Watoto
Vifaa vya michezo ya watoto vilivyopo Fun Retreat ni pamoja na sehemu mbalimbali za kuwaburudisha watoto wa rika tofauti. Kuna magari ya kuchezea yanayotumia umeme, uwanja wa watoto (children park) wenye mizunguko, bembea, na slaidi. Pia kuna michezo ya ndani kama arcade games ambayo huwapa watoto burudani . Vifaa hivi vimeandaliwa kwa kuzingatia usalama na starehe ya watoto.
Kidz Klub
Kidz Klub ni sehemu maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya watoto kujifunza na kuburudika wakati wa mapumziko yao. Lengo kuu ni kuhakikisha muda wa mtoto unatumika kwa manufaa, huku wakijifunza ujuzi muhimu wa maisha na kukuza vipaji vyao. Kuna shughuli mbalimbali zinazofanyika katika Kidz Klub ikiwa ni pamoja na kucheza majini (water play), michezo ya nje, sanaa na ufundi, mafunzo ya stadi za maisha, ujuzi wa mawasiliano, kucheza dansi kwa uhuru, michezo ya kuigiza, muziki, mazoezi ya mwili na ukuzaji wa afya ya mwili. Hizi zote husaidia katika ukuaji wa jumla wa mtoto kimwili, kiakili na kijamii.
Free Internet (WI-FI )
Unapokuwa Fun Retreat Moshono, Arusha, unaweza kufurahia huduma ya intaneti ya bure (Free WiFi) bila kikomo. Huduma hii inakuwezesha kuendelea kuwasiliana na wapendwa wako, kushiriki picha na matukio ya furaha, pamoja na kufurahia huduma za mtandaoni ukiwa ndani ya eneo la Fun Retreat.
Ofa Maalum
Kuna ofa maalum kwa wateja mbalimbali wa Fun Retreat, hasa kwa wale wanaopanga kufanya matukio kama sherehe, mikutano, au hafla za kifamilia. Wateja wanaweza kufanya pre-booking (uhifadhi wa mapema) na kunufaika na ofa hizi maalum kulingana na aina ya tukio. Ofa hizi hutolewa kwa vipindi maalum na zinaweza kujumuisha punguzo la bei au huduma za ziada kulingana na mpango wa tukio.
Nyumba au Chumba Cha Kupumzika (Resting Room)
Fun Retreat ina aina mbalimbali za malazi zinazokidhi mahitaji tofauti ya wageni. Kuna tents kwa wale wanaopendelea kukaa karibu na asili, executive rooms kwa wageni wanaotaka faraja ya hali ya juu, pamoja na vyumba vya familia vilivyobuniwa kwa ajili ya makundi au familia kubwa.
Kua wa kwanza Kutoa Maoni Yako
Andika Maoni yako ili kuwasaidia wengine kujifunza kuhusu biashara hii
Andika Maoni YakoFun retreat resort
Fun Retreat ni sehemu ya mapumziko na burudani iliyopo Moshono, Arusha. Eneo hili lina mandhari ya asili na mazingira tulivu, na hutembelewa na watu mbalimbali kwa ajili ya kupumzika na kufanya shughuli za burudani. Kuna bwawa la kuogelea, sehemu za kuchezea watoto, na maeneo ya wazi kwa ajili ya familia na makundi. Pia kuna huduma za chakula na maeneo ya kukaa kwa wageni wanaohitaji kutumia muda zaidi. Ni sehemu inayotumika pia kwa matukio kama sherehe na mikutano.
Tovuti
http://www.funretreat.com
Barua pepe
[email protected]
Simu
+255 622999555